MABORESHO YA MIFUMO YA NDANI YA UENDESHAJI WA SHUGHULI ZA OFISI

Kwa wafanyakazi wetu wote na umma kwa ujumla,

Kutokana na maamuzi yaliyotolewa na Bodi ya Ushauri katika mkutano mkuu wa mwaka uliofanyika tarehe 23/07/2020.

Uongozi wa kampuni ya Moyo Media inawataarifu wafanyakazi wake wote kwamba “Kila mfanyakazi wa Moyo Media Company Limited atatakiwa kuwasilisha taarifa zake binafsi upya, taarifa hizo ni pamoja na vivuli vyake vya elimu/taaluma/mafunzo mengine, kitambulisho cha U-Zanzibar/Taifa/Passport etc. Vivuli vyote lazima viwe vimethibitishwa uhalali wake.”

Wafanyakazi wafuatao hawatahusika kwa kuwasilisha taarifa zao:-

JINA LA MFANYAKAZI           MAHALA/OFISI
         FARID S. HUMUD               PEMBA
         JUNIOR IBRAHIM BAICE              DODOMA

Taarifa zote zitumwe kwa njia ya Posta tu na mwisho wa kupokea maombi ni tarehe  29/12/2020 na mfanyakazi yoyote atakaeshindwa kuwasilisha taarifa zake kwa wakati atahesabiwa kama si mfanyakazi wa kampuni.

Taarifa zote zitumwe kwa:

Afisa Mtendaji Mkuu,

Moyo Media Co. Ltd

P. O.  Box 271

74205 Kichungwani

Chake –Chake,

South – Pemba.

Tanzania

Pamoja na taarifa hii tunautaarifu umma kwamba hivi karibuni, In Shaa Allah tunatarajia kutangaza nafasi mpya za ajira kwa Pemba na Dodoma kwa kupitia mtandao wa Pemba Live kwa anuani ya www.pembalive.info

Imetolewa na

Afisa Mtendaji Mkuu, Moyo Media Co. Ltd